TAMKO LA UMOJA WA WABUNGE KUHUSU UJANGILI NCHINI

Kamati Tendaji ya Umoja wa Wabunge wa Uhifadhi na Matumizi Endelevu ya Wanyamapori iliyoketi mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti wake, Rizi... thumbnail 1 summary
Kamati Tendaji ya Umoja wa Wabunge wa Uhifadhi na Matumizi Endelevu ya Wanyamapori iliyoketi mjini Dodoma chini ya Mwenyekiti wake, Riziki Saidi Lulida, kuchambua sheria ya uhifadhi ya wanyamapori ya mwaka 2009 inapenda kuufahamisha umma kuwa imebaini Tanzania inapaswa kutumia njia tatu ambazo zitasaidia kudhibiti ujangili. Njia hizo ni hizi zifuatazo.



1 - Taifa linapaswa kudhibiti masoko yanayotumika kwa biashara haramu ya nyara za Taifa.



2- Taifa linapaswa kudhibiti njia za kusafirisha nyara za Taifa.



3- Taifa linapaswa kudhibiti uwindaji haramu katika hifadhi na ili kudhibiti ujangili ni lazima tuwe na “comprehensive doctrine, strategy, tactics.”

Katika uchambuzi wa tatizo la msingi la ujangili hapa nchini, kamati ilibaini kuwa ujangili ni sawa na mchezo wa PAKA na PANYA. “We need the right cats.” Ili kuondoa tatizo la ujangili, taifa linahitaji “comprehensive, intelligent and pragmatic doctrine that addresses all the problems and offers objective and inexpensive solutions, preferably using local resources and personnel.



Hata hivyo, ili kufikia mkakati wa kukabiliana na tatizo la ujangili nchini kamati ilibaini kuwa kama taifa tunahitaji kuainisha maeneo ambayo tunaweza kuwaona au kuwapata majangili na ili kufanikisha hili tunahitaji, Pro-active Investigators” (Expert Investigators are needed.)



Investigations can be both pro-active are reactive.



Proactive, should go hand in hand to benefit people ambao ni muhimu katika harakati za kulinda wanyamapori (Wananchi ndiyo walengwa katika mkakati huu.)





The community has to be engaged to assist efforts and most if at all possible benefit from the tourism and other revenue and prestige earnings and job creating activities.



Iwapo hili litafanyika, Wananchi watashiriki kuonyesha maeneo wanayojificha majangili na hii ni kwa sababu majangili huhitaji msaada wa Wananchi kupata silaha, chakula, maji na zana nyingine za kufanikisha ujangili.



Pia hutumia Wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka hifadhi kubeba nyara mbalimbali za Taifa (pembe, ngozi, kucha, n.k. hivyo Wananchi ni chanzo muhimu cha kupata taarifa mahsusi za mienendo ya majangili ndani na nje ya maeneo ya hifadhi. Hivyo, wachunguzi au scouts, rangers waliofunzwa mambo ya uchunguzi wanaweza kukusanya taarifa kutoka kwa Wananchi kuhusu “Previous Poaching Activities.



Tatizo jingine linalohitaji kushughulikiwa ni namna ya kuwasaka majangili baada ya kupata taarifa ya mienendo yao, maeneo wanayoyatumia au kujificha. Hili linahitaji ufuatiliaji ambao husaidia kuelewa mapito ya majangili sawa na namna wafugaji wanavyoweza kuelewa mienendo ya wanyama wakali.



Kamati inaamini kuwa bila shaka ziko droves ambazo zinaweza kuruka chini kwa chini na kufanya kazi nzuri lakini gharama yake ni kubwa sana hivyo ni jambo zuri tutumie wananchi kupambana na ujangili.



Tatizo jingine lililooneaka ni namna ya kuwakamata majangili. Ni vigumu na ni hatari kwa anayefuatilia mwenendo wa jangili anapomuona kumkamata mara moja kwa sababu jangili anaweza kujihami hivyo kuweka mazingira magumu ya kumkamata.



WAJIBU WA WANANCHI



Kamati inapenda kuufahamisha umme wa Watanzania kuwa Ibara ya 4 ya Sheria hii inatamka kuwa wanyamapori wote nchini Tanzania ni mali ya Umma na watakuwa chini ya dhamana ya Rais kwa niaba ya Watanzania.



Pili, Ibara 4 (2 – 6) inaelekeza utaratibu kwa mtu au watu binafsi kumiliki mnyama au wanyama.



Na inawakumbusha wananchi wote kuwa malengo makuu ya Sheria ya Uhifadhi wa Wanyamapori ni kuendeleza rasilimali za wanyamapori kwa maendeleo ya uchumi na ustawi wa maisha ya Watanzania na kutunza sekta ya utalii kwa vizazi vya sasa na vijavyo.



Ibara 15 (1) inakataza mtu yeyote asiyehusika kuingia katika maeneo ya uhifadhi isipokuwa wasafiri wanaopita kwa usafiri wa magari kwenye mbuga au boti kwenye maziwa n.k na Ibara ya 15 (2)       inatoa adhabu kwa anayevunja katazo 15 (1) kama anapatikana na hatia atatozwa faini isiyopungua Tshs.100,000 na isiyozidi Tshs. 500,000.



Aidha Ibara 17 (1) inakataza mtu kumiliki silaha, upinde, mishale na aina nyingine ya silaha ndani ya pori la akiba na Ibara ya 17 (2) inatoa adhabu kwa anayevunja maelekezo ya Ibara 17 (1) ambayo haitazidi Tshs 200,000 au kifungo cha miaka mitatu jela au vyote.

                 

Pia Ibara 20 (1)  inakataza mtu kufanya shughuli yeyote katika maeneo ya hifadhi ikiwemo kuchimba au kukusanya mchanga, madini n.k na Ibara 26 (1) fasili (1) inakataza mtu yoyote kufanya shughuli za uwindaji isipokuwa kwa ruhusa maalumu.



Watanzania wanapaswa kukumbuka kuwa wakati wa uhuru, Tanzania ilifanikiwa sana katika uhifadhi wa wanyamapori kwa sababu ya sera thabiti zilizotungwa chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere.



Katika moja ya matamko yake, Mwalimu Nyerere alipata kueleza kwa lugha ya kiingereza kuwa, “The survival of our wildlife is a matter of grave concern to all of us in Africa. These wild creatures amid wild places they inhabit are not only important as a source of wonder and inspiration but are an integrate part of our natural resources and of our future livelihoods and well being”.



Na aliwahi pia kusema ni jukumu la Watanzania kuhakikisha kwamba rasilimali za wanyamapori zinanufaisha Watanzania na watoto wa wajukuu wao. Hivyo, jukumu la kulinda wanyamapori ni la Watanzania wenyewe siyo Askari Pori “Game Rangers au Police na madhara yatokanayo na uharibifu wa rasilimali ya wanyamapori haitaathiri Tanzania peke yake bali Bara lote la Afrika na Dunia kwa ujumla wake.



Umma wa watanzania unapaswa kufahamu kuwa matatizo makuu yanayokabili uhifadhi hapa nchini ni kuwepo kwa sera dhaifu inayoshindwa kuainisha majukumu ya Wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka hifadhi na Mapori ya Akiba.



Na pamoja na mambo mengine mengi ya msingi, ufinyu wa bajeti na watendaji unasababisha Serikali kushindwa kuwashirikisha Wananchi wanaoishi Vijijini kushiriki masuala ya uhifadhi.



Kamati pia imebaini upungufu katika sera ya Uhifadhi wa Wanyamapori. Kwamba Sera imeshindwa kuonyesha namna watakavyoshirikishwa Wananchi wanaoishi maeneo yenye hifadhi na yanayozunguka Mapori ya Akiba watakavyoshirikishwa katika majukumu ya uhifadhi.



Sambamba na hilo, pia Wananchi hawajapewa elimu sahihi inayoonesha umuhimu wa wanyamapori kwa uchumi wao na Taifa na Sera imeshindwa kuonyesha mbinu na mikakati au mipango ya kuondoa au kupunguza ugomvi kati ya wafugaji, wakulima na Hifadhi za Taifa.





Riziki Said Lulida (MB)

MWENYEKITI

TANZANIA PARLIAMENTARY GROUP ON SUSTAINABLE NATURAL RESOURCES CONSERVATION AND UTILIZATION (TPGSNRCU)