Mrisho Mpoto na Peter Msechu watoa wimbo mpya wa kupinga ujangili

February 9 mwaka huu, gazeti la Daily Mail la Uingereza liliandikia kuwa “ Tanzania inaua tembo zaidi ya 11,000 kwa mwaka kwaajili ya biash... thumbnail 1 summary
February 9 mwaka huu, gazeti la Daily Mail la Uingereza liliandikia kuwa “Tanzania inaua tembo zaidi ya 11,000 kwa mwaka kwaajili ya biashara ya pembe za ndovu na Rais wake amefumbia macho’

Lilidai kuwa theluthi ya pembe zote za ndovu zinazokamatwa barani Asia hupitia Tanzania na kila siku tembo 30 huuliwa ambao ni sawa na tembo 11,000 kila mwaka. Habari hiyo iliipa Tanzania sifa mbaya hali ambayo imewasukuma Mrishi Mpoto na Peter Msechu kutumia sauti zao kukemea mauaji tembo na vifaru.
f4b7e9a4b98511e3a6680e0368da678b_8 Mrisho Mpoto na Peter Msechu wakiongea na waandishi wa habari
Wasanii hao waliokuwa na mkutano na waandishi wa habari leo, wameungana kuanzisha kampeni yao ya kupambana na ujangili dhidi ya tembo na vifaru.

“Tumeachia wimbo mpya na video yake unaoitwa DENI LA HISANI pia tumerelease rasmi tshrt zetu zinazoitwa USINIUE NITUNZE… Tunawaomba wote tuungane kwa pamoja tupinge mauaji dhidi ya wanyama wasio na hatia,” ameandika Peter Msechu kwenye Instagram.