Uwanja
wa ndege wa Changi wa Singapore umeibuka kinara na kubeba kwa mara ya
pili tuzo ya uwanja bora zaidi wa ndege duniani kati ya viwanja 410
vilivyopigiwa kura na wasafiri zaidi ya milioni 12 na laki 8.
Kwa mujibu wa tovuti maalum ya tuzo hizo zilitolewa jijini Barcelona, Hispania. Mwaka jana uwanja huo ulishinda tuzo hiyo pia.
“Kushinda
tuzo hii ya thamani kwa mara ya pili inaonesha kuwa Changi inaonesha
kuwa ni zaidi ya uwanja wa ndege.” Amesema Edward Plaisted, CEO wa
shirika la Skytrax la Singapore.
Tuzo
hiyo hutolewa kwa kukusanya kura za wasafiri wa nchi 110 duniani kote
na huzingatia ubora wa uwanja na huduma zinazotolewa kwa wasafiri.
Hiii ni orodha ya viwanja vya ndege kumi bora zaidi kwa mujibu wa tuzo hizo:
- Singapore Changi Airport
- Incheon International Airport
- Munich Airport
- Hong Kong International Airport
- Amsterdam Schiphol Airport
- Tokyo International Airport Haneda
- Beijing Capital International Airport
- Zurich Airport
- Vancouver International Airport
- London Heathrow Airport