Maonyesho ya utalii Oktoba

Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii (TTB) imeandaa Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii yatakayokuwa yakifanyika kila mwaka ... thumbnail 1 summary
Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Bodi ya Utalii (TTB) imeandaa Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii yatakayokuwa yakifanyika kila mwaka kuanzia mwaka huu.
 
Akizindua tovuti ya maonyesho hayo yanayotarajiwa kuanza Oktoba 1-4 mwaka huu jijini hapa, Waziri Lazaro Nyalandu alisema Serikali imejipanga kuhakikisha sekta hiyo inawanufaisha wananchi zaidi.
“Nitahakikisha tunawaalika mawaziri na mawakala wa utaliikutoka nchi mbalimbali washirika wetu duniani. Tunatarajia maonyesho haya yawe makubwa na yaitangaze Tanzania kama kituo muhimu cha utalii duniani,” alisema Nyalandu.
Maonyesho hayo yatakayojulikana kama Swahili International Tourism Expo (Site), yanatarajiwa kupanua wigo wa utalii nchini hasa kwa kuvitangaza vivutio vya maeneo mengine ya nchi, hasa kusini baada ya upande wa kaskazini kufanya vizuri.