Changamoto katika sekta ya utalii Mkoani Lindi na mbinu za kukabiliana nazo

Ili utalii uweze kuendeshwa katika mkoa huu kunahitajika mambo kadhaa kama, Miundo mbinu ya mawasiliano, mahoteli ya kisasa, usafiri wa ang... thumbnail 1 summary
Ili utalii uweze kuendeshwa katika mkoa huu kunahitajika mambo kadhaa kama, Miundo mbinu ya mawasiliano, mahoteli ya kisasa, usafiri wa anga wan chi kavu na bahari na wakazi wake kuwa tayari kuwapokea watalii na kufanya kazi vizuri katika maeneo ya huduma za kitalii. Baadhi ya huduma hizo Serikali kuu imetoa kwa mfano ujenzi wa daraja la Mkapa na ujenzi wa barabara ya Mingoyo Lindi Kibiti ambao unaendelea.

Mahoteli na nyumba za kulala wageni
Miji ya mkoa huu haina hoteli za kutosha na za kisasa vivutio vya Utalii. Lindi mjini hakuna Hoteli ya Kitali. Zilizopo hazipo katika “Standard” ya juu. Hazina uchaguzi wa chakula maji yake ya kuchota nay a shida umeme nao sio wakuaminika. Hali hii pia imeikumba wilaya ya Liwale. Kilwa kuna hoteli chache zinazotoa huduma kwa Watalii.

Usafiri
Hakuna usafiri wa kuamnika toka Dar es Salaam hadi Kilwa, Lindi na Liwale. Safari tours zinahitajika. Panatakiwa pia usafiri wa boti toka Kilwa masoko kwenda Kilwa Kisiwani halikadhalika wa kwenda songo Mnara.
Usafiri wa anga na viwanja vya ndege

Kiwanja cha ndege cha Kikwetu cha Lindi mjini ni kizuri na kinatumika hata kwa ndege kubwa. Kinachotakiwa ni huduma ya usafiri toka uwanjani kuja mjini Lindi.
Uwanja wa Kilwa ni mdogo tena upo katikati ya mji. Uwanja mpya unatakiwa ujengwe nje kidogo ya mji (Maoni ya mwandishi).
Vivutio vya mafuta.


Kunahitajika vituo vingi vya mafuta mjini Lindi, Nangurukuru, Kilwa na Liwale. Pia ni busara kuwa na kituo cha mafuta kati ya Nangurukuru na Liwale, ingefaa Njinjo kungejengwa kituo hicho. Vituo vichache vya mafuta vilivyopo vinaendeshwa na matajiri wenye mitaji midogo na mara kwa mara huishiwa mafuta.