Sanamu ya Mandela kuzinduliwa Marekani

Sanamu kubwa ya Rais wa zaman wa Afrika Kusini Nelson Mandela inazinduliwa rasmi septemba 21 mwaka huu huko Washington kwenye eneo ambalo... thumbnail 1 summary
Sanamu kubwa ya Rais wa zaman wa Afrika Kusini Nelson Mandela inazinduliwa rasmi septemba 21 mwaka huu huko Washington kwenye eneo ambalo maelfu ya wamarekani walikusanyika kushinikiza kuachiwa kwa Mandela kutoka gerezani na uhuru wa Afrika ya Kusini kutoka mikononi mwa makaburu.

Sanamu hilo lenye urefu wa futi sita limetengenezwa na mchonga vinyago Jean Doyle na litawekwa nje ya ubalozi wa Afrika Kusini Marekani uliopo kwenye jimbo la Massachusetts.
Sanamu hilo imetengenezwa kwa mfano wa picha aliyowahi kupiga Mandela wakati wa kutangaza harakati za uhuru nchini humo Febriari 11, 1990.
Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa, Maite Nkoana-Mashabane na mwenyekiti wa African National Congress (ANC) Baleka Mbete watakuwa miongoni mwa watakaoiwakilisha Afrika Kusini kwenye tukio hilo.

Maofisa kutoka ikulu ya Marekani nao watakuwepo.