Afisa
Msaidizi wa Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA),Eva Mallya
akitoa maelezo kwa Warembo wanaowania Taji la Redd's Miss Tanzania
2012,juu ya Utaratibu wa Upandaji Upandaji wa Mlima Kilimanjaro.Warembo
hawa walitembelea eneo hilo la Mwanzo wa Mlima Kilimanjaro uliopo
Marangu kwa ajili ya kujifunza mambo mbali mbali ya utalii wa ndani.
Baadhi
ya Warembo wanaowania taji la Redd's Miss Tanzania 2012 wakizungumza
na baadhi ya wabeba Mizigo ya Watalii mbali mbali waliofika kwenye
Lango kuu la Kupanda Mlima Kilimanjari,lililopo Marangu Mkoani
Kilimanjaro.Warembo hawa wametembelea eneo hilo la Mwanzo wa Mlima
Kilimanjaro uliopo Marangu kwa ajili ya kujifunza mambo mbali mbali ya
utalii wa ndani.
Baadhi ya Warembo wakiwa Wamebeba Mabegi mithili ya Watalii wanaopanda mlima Kilimanjaro.
Baadhi
ya Warembo wa Redd's Miss Tanzania wakiwa kwenye picha ya Pamoja na
Baadhi ya Watalii waliokuwa wakirudi kutoka mlima Kilimanjaro.
Warembo katika pozz
Warembo wakiwa kwenye picha ya Pamoja.
Warembo wakiondoka eneo hilo la Mwanzo wa Upandaji wa Mlima Kilimanjaro.
Chanzo: Dar es Salaam Yetu