LEO JUMAPILI USIKU USIKOSE KUANGALIA MWEZI UKISOGEA ANGANI

Na Dkt  Noorali T. Jiwaji Leo Jumapili tarehe 8 Septemba, upande wa magharibi karibu na upeo, utauona Mwezi ukiosogea nafasi y... thumbnail 1 summary


Na Dkt Noorali T. Jiwaji
Leo Jumapili tarehe 8 Septemba, upande wa magharibi karibu na upeo, utauona Mwezi ukiosogea nafasi yake angani mbele ya macho yako, ukiuangalia kwa saa moja hivi kuanzia baada tu ya machweo, hadi baada ya saa mbili hivi. (angalia picha chini)

Nyota ya Spika inayoonekana kushoto wa Mwezi mwandamo ipo juu kidogo tu ya Mwezi, lakini baada tu ya saa moja hivi utaona nyota ya Spika iko chini kidogo ya Mwezi mwandamo.

Kilichotokea kihalisi ni kwamba kwa vile Mwezi unatembea kwa kasi kubwa katika mzunguko wake wakati nyota hasizogei, kihalisi, ni Mwezi uliosogea kupanda juu.

Sayari zote, pamoja na Mwezi, husogea kutoka magharibi kwenda mashariki ukilinganisha na nyota, ambazo hazisogei angani kwa vile zipo mbali mno na sisi.


Nyota angavu sana inayoonekana juu ya Mwezi si nyingine ila 'nyota ya jioni' ambayo ni sayari ya Zuhura.  Mwezi mwandamo na nyota angavu ya Zuhura inatoa mandhari ya kuvutia sana angani.