Warsha ya ufuatiliaji na tathmini ya kitaifa ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi yafunguliwa rasmi Kibaha

--------------------------------------------------------------------- Evelyn Mkokoi, Afisa Habari ofisi ya Makamu wa Rais Kibaha.... thumbnail 1 summary


---------------------------------------------------------------------
Evelyn Mkokoi, Afisa Habari ofisi ya Makamu wa Rais

Kibaha.
Ufuatiliaji na tathimini ya kitaifa ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi ni njia mojawapo itakayoisaidia Tanzania katika juhudi za pamoja za dunia za kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.
Hayo yameelezwa leo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Sazi Salula wakati wa ufunguzi wa Warsha ya ufuatiliaji na tathmini ya kitaifa ya kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.
“Wote tumeshuhudia madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi, yaliyojitokeza nchini kwetu ikiwa ni pamoja na mvua kubwa zilizonyesha miaka ya hivi karibuni zilizosababisha mafuriko, hali ya ukame, na uhaba wa chakula” alisema Salula
Salula amesema madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi yana athiri nchi na dunia kwa ujumla lakini nchi zilizo maskini zaidi duniani huathirika kwa kiasi kikubwa zaidi.
Alisema kuwa anaamini warsha hiyo itasaidia kupatikamna kwa kablasha ambalo litakuwa na umuhimu kw ataifa hili kwani litasaidia ufuatiliaji na tathmini katika suala zima la kuhimili mabadiliko ya tabia nchi.